Friday, July 25, 2014

VAN GAAL ANAFANANA NA FERGUSON - GIGGS.

KOCHA msaidizi wa klabu ya Manchester United, Ryan Giggs amesema kocha mpya wa timu hiyo Louis van Gaal kuna baadhi ya mambo yake anafanana na Sir Alex Ferguson. Mholanzi huyo alisimama kama kocha wa United kwa mara ya kwanza jana na kuchuhudia kikosi hicho kikiicharanga Los Angeles Galaxy kwa mabao 7-0 katika mchezo wa kirafiki wa maandalizi ya msimu mpya uliochezwa Marekani. Van Gaal anajulikana kwa kushinda mataji akiwa na vilabu vya Ajax Amsterdam, Bayern Munich na Barcelona katika kipindi chake cha ukocha na Giggs hashangazwi na mafanikio hayo. Akihojiwa Giggs amesema kuna baadhi ya vitu makocha hao wawili wanashabihiana akimaanisha Van Gaal na Ferguson huku akiongeza kuwa wote wanapenda wachezaji kujitoa na kuwa na heshima. Giggs aliendelea kudai kuwa Van Gaal anataka kila kitu kwenda sawa mwanzoni mwa mazoezi hadi mwisho kitu ambacho hata Ferguson alikuwa nacho.

No comments:

Post a Comment