Friday, July 25, 2014

GYAN AJITIA KITANZI AL AIN.

NAHODHA wa timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan ameongeza mkataba wake na klabu ya Al Ain ya Falme za Kiarabu ambao unamalizika mwaka 2018. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Sunderland alikuwa amebakisha mkataba wa miaka mwili na nusu lakini aliongezwa mkataba mwingine ulioboreshwa zaidi jana. Gyan mwenye umri wa miaka 28 amekuwa mfungaji anayeongoza katika Ligi Kuu ya huko kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo. Nyota huyo ambaye alijunga na Al Ain akitokea Sunderland kwa mkopo mwaka 2011, amefunga mabao 82 katika mechi 66 za ligi alizocheza.

No comments:

Post a Comment