Thursday, July 31, 2014

MECHI YA LIGI YA MABINGWA ULAYA YASIMAMISHWA KWA SABABU YA VURUGU.

VURUGU baina ya mashabiki mahasimu zimesababisha kukosekana amani kwa dakika 15 katika mhcezo wa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya kati ya Dnipro Dnipropetrovsk na FC Copenhagen uliochezwa katika Uwanja wa Olimpiysky jijini Kiev jana. Mashabiki wa FC Copenhagen wa Denmark walishambuliwa na kundi la watu wasiojulikana wanaoaminika kuwa mashabiki wa Dnipro na kulazimika kutafuta mahali pa kujificha katika majukwaa huku mwamuzi Andre Marriner akichelesha mchezo kuanza katika kipindi cha pili kwa dakika 15 zaidi. Tayari viongozi wa Fc Copenhagen wameshatuma barua ya malalamiko kwa Shirikisho la Soka barani Ulaya mara baada ya mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bila kufungana. Hata hivyo mmoja wa wawakilishi wa mashabiki wa Dnipro ametuhumu mashabiki wa Denmark kwa kuamsha vurugu hizo kwa kupeperusha bendera ya urusi. Serikali ya Ukraine inapambana na waasi wanaotaka kujiunga na Urusi mashariki mwa nchi hiyo baada ya Crimea kufanya hivyo machi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment