Wednesday, August 27, 2014

AFCON 2015: EBOLA YAZIDI KULETA BALAA, CONGO YAGOMA KWENDA NIGERIA.

SHIRIKISHO la Soka nchini Nigeria-NFF limedai kuwa halijapata taarifa yoyote rasmi kutoka Shirikisho la Soka la Afrika-CAF juu ya madai ya Congo Brazzaville kuelekea katika mchezo wao kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika utakaofanyika huko Calabar. Congo ambao watakuwa wageni wa Nigeria katika mchezo huo utakaochezwa Septemba 6 mwaka huu wametuma malalamiko CAF kueleza wasiwasi wao juu usalama katika mchezo huo. Congo wamesisitiza hawatakwenda katika mji wa Calabar au mji mwingine wowote nchini Nigeria kwa ajili ya mcjhezo huo kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa Ebola. Kumeguwa na wagonjwa wengi walioripotiwa katika baadhi ya sehemu za mji wa Liberia, Guinea, Sierra Leone na Nigeria ambavyo vifo vya watu 1,427 vimeripotiwa huku wengine zaidi ya 2,615 wakiambukizwa toka ugonjwa huo ulipolipuka Machi mwaka huu. Kocha wa timu ya taifa ya Congo, Claude Leroy amesema itakuwa ngumu na hatari kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo huo na kudai kuwa hata majirani zao Cameroon tayari wamefunga mipaka yao ili kuepusha maambukizi zaidi. Hata hivyo NFF wamesisitiza kuwa mchezo utafanyika kama ulivyopangwa katika Uwanja wa UJ Esuene uliopo mji wa Calabar.


No comments:

Post a Comment