Wednesday, August 27, 2014

PAMOJA NA KIPIGO CHA FEDHEHA, VAN GAAL ADAI HAJUTII CHOCHOTE.

KLABU ya Manchester United, Louis van Gaal amesema hana cha kujutia kutokana na mbinu na kikosi alichotumia jana kilichofungwa na timu ya MK Dons na kuondolewa katika michuano ya Kombe la Ligi. United walichapwa mabao 4-0 na timu hiyo ya daraja la pili yaliyofungwa na Will Grigg na Benik Afobe anayecheza kwa mkopo akitokea Arsenal, na kumuacha Van Gaal bila ushindi katika mechi tatu alizocheza toka akalie nafasi hiyo. Hata hivyo, Van Gaal hakuomba radhi kutokana na kipigo hicho na kusisitiza kuwa alikuwa sahihi kuchagua kikosi kilichotawaliwa na vijana na wachezaji wasio na uzoefu. Akihojiwa Mholanzi huyo amesema hajutii chochote kutokana na kupoteza mchezo huo kwani alipanga kikosi sahihi na mbinu alizotumia zilikuwa nzuri ila bahati haikuwa upande wao. Ila pamoja na hayo Van Gaal aliwaomba mashabiki wa klabu hiyo kuwa subira na kudai kuwa anahitaji muda ili kuigeuza timu hiyo kuwa ya ushindi.

No comments:

Post a Comment