Wednesday, August 27, 2014

DI MARIA AWAAMBIA MASHABIKI WA MADRID KUWA HAKUONDOKA KWA MAPENZI YAKE.

WINGA mpya wa klabu ya Manchester United, Angel Di Maria ameandika barua ya wazi kwa mashabiki wa Real Madrid akidai kuwa hakutaka kuondoka kwa wakongwe hao wa soka nchini Hispania. Nyota huyo alikamilisha usajili wake uliogharimu paundi milioni 60 jana huku United wakimpa mkataba wa miaka mitano. Lakini mwenyewe amesisitiza kuwa alikuwa yuko tayari kusaini mkataba mpya na mabingwa hao wa soka barani Ulaya. Katika barua yake iliyochapishwa katika gazeti la Marca la Hispania, Di Maria amesema anatakiwa kuondoka lakini anataka kuweka wazi kuwa haikuwa nia yake kufanya hivyo. Nyota huyo aliendelea katika barua hiyo kuwa baada ya kushinda taji la Ligi ya Mabingwa alikwenda katika Kombe la Dunia akiwa na matumaini ya kupewa mkataba lakini jambo hilo halikufanyika. Di Maria amesema kuna mambo mengi anayothamini na mengi kati ya hayo hayahusiani na masuala ya mshahara, ni mategemeo yake ataendelea kukua akiwa United moja ya klabu kubwa duniani na ana matumaini ya kuandika historia mpya akiwa hapo.

No comments:

Post a Comment