Wednesday, August 27, 2014

KUFUNGWA ILIKUWA HALALI - KOCHA CELTIC.

MENEJA wa klabu ya Celtic Ronny Deila amesema kikosi chake hakikuwa fiti baada ya kutandikwa bao 1-0 na Maribor ya Slovenia na kujikuta wakishindwa kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na Marcos Tavares akitumia vyema udhaifu wa mabeki na kuifanya Celtic kuangukia katika michuano ya Europa Leauge. Akihojiwa Deila amesema hawakufungwa kwasababu ya mabeki bali wamepoteza mchezo huo kwasababu wameshindwa kutengeneza nafasi za kufunga hivyo ni mategemeo yao watasimama katika nafasi hiyo msimu ujao. Mechi za kufuzu hatua ya makundi zinaendelea tena leo ambapo Arsenal watakuwa wenyeji wa Besiktas ya Uturuki katika Uwanja wa Emirates.

No comments:

Post a Comment