Wednesday, August 27, 2014

BAYERN YATAKA KUSAJILI KINGA LA MONCHENGLADBACH.

MWENYEKITI wa klabu ya Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge ameiambia klabu ya Borussia Monchengladbach kukubali ofa yao kwa ajili ya Sinan Kurt au wahatarishe kumkosa kinda huyo kwa kusajiliwa kama mchezaji huru katika usajili wa kiangazi mwakani. Mabingwa watetezi wa Bundesliga wamepania kumsajili chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 18 lakini wameshindwa kufikia makubaliano ya klabu yake hiyo. Katika siku za karibuni Kurt amesema anataka kuendeleza soka lake Bayern ingawa klabu hiyo iko tayari kusubiri kwa mwaka mzima kama klabu yake itakataa kushusha bei wanayotaka. Rummenigge amesema mkurugenzi wa Monchengladbach, Max Eberl anataka fedha zaidi kuliko walizoahidi wakurugenzi wake Matthias Sammer na Michael Reschke. Mwenyekiti huyo aliendelea kudai kuwa hali hiyo ni ya kawaida lakini mkataba wa mchezaji unamalizika mwakani hivyo hawatakiwi kusahau kuwa kama wakikwamisha uhamisho huo mchezaji huyo anaweza kuondoka bure.

No comments:

Post a Comment