Wednesday, August 27, 2014

MADRID WAMEPANIA KUWEKA HISTORIA - BALE.

WINGA mahiri wa Real Madrid, Gareth Bale amesisitiza kuwa wana nia ya kuweka historia na kuwa klabu ya kwanza kutetea taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya. Madrid waliitandika Atletico Madrid kwa mabao 4-1 baada ya muda wa nyongeza msimu uliopita na kushinda taji lao la 10 la michuano hiyo na nyota huyo wa zamani wa tottenham Hotspurs ana hamu ya kuongeza mataji zaidi katika msimu huu wa 2014-2015. Akihojiwa Bale amesema kushinda taji la 10 la Ulaya lilikuwa jambo bora kwa kila mtu na kufunga bao katika mchezo wa fainali ilikuwa ni moja kati ya ndoto zake hgivyo anadhani msimu uliopita ulikuwa mzuri kwao. Bale amesema kwasasa wanatakiwa kuangalia ya mbele na kujaribu kushinda taji hilo tena na kwa kufanya hivyo watakuwa wameweka historia ya kipekee. Madrid walianza vyema kwa kuichapa Sevilla mabao 2-0 mapema mwezi huu katika mchezo wa Super Cup ya Ulaya lakini walijikuta wakichapwa jumla ya mabao 2-1 na mahasimu wao Atletico katika mchezo wa ngao ya jamii kufunga pazia la La Liga.

No comments:

Post a Comment