Wednesday, August 27, 2014

WENGER AMKINGIA KIFUA SANCHEZ.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amemkingia kifua Alexis Sanchez kwa kiwango bora alichoonyesha katika nafasi ya mshambuliaji wa kati katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Everton uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 Jumamosi iliyopita. Arsenal walipambana kutoka nyuma kwa mabao 2-0 na kuhakikisha wanapata sare katika Uwanja wa Goodison Park ingawa nyota huyo aliyesajiliwa kwa euro milioni 42 msimu huu alitolewa baada ya mapumziko na nafasi yake kuchukuliwa na Olivier Giroud. Kuelekea katika mchezo wao wa leo dhidi ya besiktas katika Uwanja wa Emirates, Wenger amesema anadhani Sanchez alicheza vyema katika mchezo wa Jumamosi lakini bado anahitaji muda ili aweze kuzoea mikikimikiki ya ligi hiyo. Pamoja na Giroud kuumia katika dakika za mwisho za mchezo huo, Wennger amesema hana shaka katika hilo kwani ana washambuliaji wa kutosha katika kikosi chake. Arsenal walitoka sare ya bila ya kufungana na Besiktas katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliochezwa huko Instabul ikiwa ni mara ya kwanza kushindwa kushinda mechi za hatua hiyo mtoano ili waweze kufuzu makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment