Wednesday, August 27, 2014

BAADA YA DI MARIA SASA MAN UNITED WAAMUA KUKOMAA NA VIDAL.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Louis van Gaal na ofisa mkuu Ed Woodward sasa wamehamishia nguvu zao kumuwinda Arturo Vidal baada ya kumaliza kusajili Angel Di Maria jana. United imekuwa ikipinga kumuhitaji Vidal kwa kipindi kirefu kiangazi hiki lakini sasa wanadaiwa kuanza mazungumzo kama wanayoanya na Ajax Amsterdam kwa ajili ya kumsajili Daley Blind. Majeruhi ndio yalioonekana kumzuia Van Gaal kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Chile ambaye ana thamani ya paundi milioni 30 lakini kutokana na matokeo mabovu ya hivi karibuni klabu imeona hakuna jinsi bali kutumia fedha ili wajiimarishe. Upasuaji wa goti msimu uliopita ulimzuia Vidal kuitumikia Juventus toka mwishoni mwa Machi mwaka huu ingawa baadae alipona na kupata muda wa kuwepo katika kikosi cha Chile katika michuano ya Kombe la Dunia. Ujio wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 United kutasaidia kuimarisha safu ya kiungo ambayo imeonekana kuyumba na kupelekea kipigo cha mabao 4-0 jana dhidi ya timu ya daraja la pili ya MK Dons katika mcheo wa Kombe la Ligi. Kama United wakifanikiwa kumsajili Vidal watakuwa wamefikisha kiasi cha paundi milioni 150 walizotumia msimu huu kwa ajili ya usajili baada ya kufunja rekodi nchini Uingereza kwauhamisho wa Di Maria.

No comments:

Post a Comment