Thursday, August 28, 2014

REAL MADRID HAWAKUMPA HESHIMA ILIYOSTAHILI MWANANGU - BABA.

BABA yake winga mahiri Angel Di Maria ameiponda Real Madrid kufuatia uhamisho wa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina kwenda Manchester United na kucheza pendekezo la mwabingwa hao wa Ulaya kumpa ofa mwanae ya kumlipa euro milioni 6 kwa mwaka. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 aliondoka Madrid kwa dili lililogharimu euro milioni milioni 75 mapema wiki hii baada ya kukataa ofa ya kuongeza mnkataba Santiago Bernabeu ambao ungegharimu kiasi hicho kilichoripotiwa. Hata hivyo mzee huyo Miguel Di Maria amesisitiza kuwa mwanae alikuwa anadhani hathaminiki kitu ambacho amedai ndio kilichochangia kuongezswa euro milioni 1.5 katika mshahara wake. Baba yake Di Maria aliendelea kudai kuwa mwanae alikuwa amechoka kuonyesha thamani yake kwani ni jambo amekuwa akilifanya kwa kipindi kirefu lakini hakupata heshima aliyostahili. Kwasasa Di Maria anafuraha United na wanamhudumia vizuri huku mshahara wake ukizidi ule ambao angepewa na Madrid. Usajili wa Di Maria unakuwa wan ne uliotumia fedha nyingi baada ya kuwasajili pia Ander Herrera, Luke Shaw na Marcos Rojo.

No comments:

Post a Comment