Monday, August 25, 2014

ALGERIA YASIMAMISHA LIGI KUFUATIA KIFO CHA MCHEZAJI.

SHIRIKISHO la Soka nchini Algeria limesimamisha Ligi Kuu kufuatia kifo cha mchezaji wa Cameroon Albert Ebosse ambaye alipigwa na jiwe lililorushwa na mashabiki. Uamuzi huo umefikiwa jana katika kikao kilichofanyika jana. Ebosse mwenye umri wa miaka 24 alipigwa na jiwe kichwani wakati akitoka uwanjani baada ya timu yake ya JS Kabylie kufungwa na USM Alger huko Tizi Ouzou juzi. Tayari mamlaka inayohusika imeshaufungia Uwanja wa 1st Novemba 1954 kulikotokea tukio hilo. Shirikisho hilo pia limeamua kutoa ubani wa dola 100,000 kwa familia ya Ebosse kiwango ambacho kinaaminika angeweza kukipata katika kipindi cha mkataba wake huku wachezaji wa Kabylie nao wakitoa mishahara yao ya mwezi kama rambirambi ya kufariki kwa mwenzao. Imegundulika kuwa uwanja wa 1st Novemba 1954 ulikuwa katika matengenezo wakati wa mchezo huo na mashabiki walitumiwe mawe ya ujenzi yaliyokuwa yamewekwa maeneo hayo.

No comments:

Post a Comment