Monday, August 25, 2014

SUPER MARIO KULAMBA PAUNDI 90,000 KWA WIKI ANFIELD.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Italia, Mario Balotelli anatarajiwa kuanguka mkataba wa miaka mitatu katika klabu ya Liverpool baada ya leo kuelekea katika mchezo wao Ligi Kuu dhidi ya Manchester City. Kikosi cha Liverpool kinachoongozwa na Brendan Rodgers kitapata morali kwa kutangazwa kwa Balotelli kuwa mchezaji wao kabla ya kuanza kwa mchezo huo. Balotelli mwenye umri wa miaka 24 ambaye ameondoka AC Milan kwa kitita cha paundi milioni 16 alitua katika uwanja wa mazoezi wa Melwood mchana wa leo kumalizia hatua za mwisho za usajili wake. Wiki iliyopita nyota huyo alikwenda Melwood kukamilisha vipimo vya afya na kukubali mkataba huo ambao utamuwezesha kuchukua kitita cha paundi 90,000 kwa wiki. Wakati akiwa Manchester City Balotelli alifanikiwa kufunga mabao 30 katika mechi 80 alizocheza huku akifunga mabao 18 katika mechi 41 alizoichezea Milan msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment