Monday, August 25, 2014

UJERUMANI WANAWAKE NAO WANYAKUWA KOMBE LA DUNIA.

TIMU ya taifa ya wanawake ya Ujerumani imefanikiwa kunyakuwa Kombe la Dunia kwa wachezaji wanawake wenye umri chini ya miaka 20 kwenye michuano iliyokuwa inafanyika huko Montreal, Canada. Ujerumani walifanikiwa kuwazidi maarifa Nigeria katika mchezo wa fainali kwa kuwafunga bao 1-0 kama ilivyokuwa kwa timu ya wanaume iliyonyakuwa taji hilo katika michuano iliyofanyika nchini Brazil. Pamoja na kuonyesha mchezo mzuri huku wakimiliki vyema mpira, Nigeria walishindwa kabisa kupenya ngome ngumu ya wapinzania wao. Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na Lena Petermann ambaye alifunga katika dakika ya nane ya muda wa nyongeza baada ya timu hizo kushindwa kufungana katika muda wa kawaida. Mshambuliaji wa Nigeria na mfunmgaji bora wa mashindano hayo Asisat Oshoala alikosa nafasi kadhaa za wazi wakati golikipa wa Ujerumani Meike Kamper alitajwa kama mchezaji bora wa mechi hiyo.

No comments:

Post a Comment