Monday, August 25, 2014

RONALDO FITI KUIKABILI CORDOBA.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo anaweza kuanza katika mchezo wa ufunguzi wa La Liga dhidi ya timu iliyopanda daraja ya Cordoba pamoja na kushambuliwa na majeruhi. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno alitokea benchi katika mchezo wa Super Cup uliochezwa Ijumaa iliyopita na kufungwa na Atletico Madrid. Meneja wa Madrid Carlo Ancelotti amesema Ronaldo amefanya mazoezi vyema hivyo anaweza kumpanga katika kikosi chake. Ancelottio alikiri kuwa wakati wa maandalizi ya msimu alikuwa akisumbuliwa na majeruhi hivyo anahitaji kufanya jitihada ili aweze kurejea katika kiwangop chake. Ronaldo mwenye umri wa miaka 29 ambaye anashikilia tuzo ya mchezaji bora wa dunia alipata majeruhi ya mgongo wakati timu hizo mbili zilipotoa sare ya bao 1-1 katika mchezo wa mkondo wa kwanza.

No comments:

Post a Comment