Tuesday, August 26, 2014

BRENDAN RODGERS AMTAHADHARISHA BALOTELLI KUWA HIYO NI NAFASI YAKE YA MWISHO.

MENEJA wa klabu ya Liverpool, Bredan Rodgers amedai kuwa Mario Balotelli yuko katika nafasi yake ya mwisho baada ya kujiunga na Liverpool kwa kitita cha paundi milioni 16. Nyota huyo wa kimataifa wa Italia mwenye umri wa miaka 24 alikuwa jukwaani akiitizama timu yake hiyi mpya ikichapwa mabao 3-1 na klabu yake ya zamani ya Manchester City Jumatatu baada ya kutoka AC Milan kwa dili la miaka mitatu. Balotelli alikuwa na matukio kadhaa yenye utata akiwa City lakini wakati Rodgers akikiri usajili huo ni wa hatari pia amedai watatumia nafasi hiyo kumkuza kama mchezaji na kumsaidia kupata ukomavu. Rodgers amesema Balotelli ni kijana mwenye upeo na akili na anajua alipo katika soka lake hivi sasa kwani nafasi hiyo inaweza kuwa ya mwisho kung’ara. Liverpool ambao walimaliza wakiwa katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu msimu uliopita nyuma ya mabingwa City kwa alama mbili, walimuuza mshambuliaji anayeongoza kwa mabao Luis Suarez kwa kitita cha paundi milioni 75 kwenda Barcelona.

No comments:

Post a Comment