Tuesday, August 26, 2014

UCHOVU WA SUPER CUP UMECHANGIA SARE YA ATLETICO - SIMEONE.

MENEJA wa klabu ya Atletico Madrid, Diego Simeone anaamini kuwa nguvu walizotumia katika mchezo wa Super Cup ziliwagharimu katika mchezo wao wa ufunguzi wa La Liga dhidi ya Rayo Vallecano ambao ulimalizika kwa sare ya bila kufungana. Mabingwa hao watetezi wa La Liga walipambana na mahasimu wao Real Madrid mara mbili katika kipindi kisichozidi siku nne na Simeone anaamini kuwa uchovu ulichangia kikosi chake kutoa sare katika mchezo huo. Akihojiwa Simeone amesema walikuwa wametoka kucheza na Madrid Jumanne na Ijumaa na nguvu walizotumia katika siku hizo zilijionyesha katika kipindi cha pili cha mchezo wa jana. Hata hivyo Simeone alilaumu kikosi chake kwa kushindwa kutumia nafasi walizopata katika kipindio cha kwanza lakini anaamini wenyeji wao hao walikuwa bora zaidi yao katika kipindi cha pili.

No comments:

Post a Comment