Tuesday, August 26, 2014

CHAMPIONS LEAGUE: ARSENAL FITI KUIZAMISHA BESIKTAS.

KIUNGO mahiri wa Arsenal, Jack Wilshere ana uhakika kuwa sare waliyopata dhidi ya Everton itawasaidia katika mchezo wao muhimu wa mtoano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Besiktas hapo kesho. Kikosi hicho kinachonolewa na Arsenal Wenger kinatarajia kuelekea katika mchezo wao huo wa mkondo wa pili wakiwa wametoshana nguvu na Waturuki hao baada ya kutoka sare ya bila kufungana katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Instabull wiki iliyopita. Hiyo inakuwa mara ya kwanza kwa Arsenal katika mechi 13 walizocheza za mtoano kushindwa kushinda. Lakini Arsenal sasa wanajisikia vyema baada ya kufanikiwa kutoka nyuma kwa kufungwa mabao 2-0 na kufanikiwa kutoa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Everton Jumamosi iliyopita. Akihojiwa Wilshere amesema alama waliyopata dhidi ya everton ilikuwa ni muhimu kwani inawapa nguvu kwa ajili ya mchezo wao wa kesho.

No comments:

Post a Comment