Tuesday, August 26, 2014

WAZIRI NDIO AMENIOMBA NIISAIDIE SUPER EAGLES - KESHI.

KOCHA Stephen Keshi amethibitisha kuwa Waziri wa Michezo wa Nigeria Tammy Danagogo amewezesha yeye kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo kwa mechi mbili za kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika dhidi ya Congo Brazzaville na Afrika Kusini. Kumekuwa na mambo mengi yanayoendelea katika uongozi wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo huku kukiwa na mipango ya kuandaa mkutanio mkuu na uchaguzi wa kamati mpya ya utendaji. Akihojiwa akiwa nyumbani kwake huko Califonia, Marekani, Keshi amesema kutokana na mambo yanayoendelea waziri amemuomba kusimamia mechi hizo mbili mpaka hapo hali itakapotulia NFF na anafurahi kuitumikia nchi yake. Toka kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil ambapo Nigeria ilitolewa katika hatua ya makundi, kumekuwa na migogoro ya hapa na pale katika NFF huku baadhi ya viongozi wake wakisimamishwa na kulifanya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kluingilia kati. Migogoro hiyo imesababisha Keshi ambaye mkataba wake ulimalizika baada ya michuano hiyo kushindwa kuanza mazungumzo ya mkataba kutokana na kutokuwa na uongozi unaoeleweka.

No comments:

Post a Comment