Tuesday, August 26, 2014

EVERTON YAMTENGEA ETO'O MKATABA WA MIAKA MIWILI.

KLABU ya Everton inakaribia kukubaliana mkataba wa miaka miwili kumsajili mshambuliaji Samuel Eto’o baada ya kuachwa na Chelsea mwishoni mwa msimu uliopita. Liverpool wamekuwa wakimtaka nyota huyo wa kimataifa wa camertoon mwenye umri wa miaka 13 lakini baada ya kukamilika kwa dili la Mario Balotelli aliyesajiliwa kwa paundi milioni 16 kunaacha njia nyeupe kwa Everton kuanza mazungumzo na Eto’o. Mazungumzo bado yanaendelea lakini Everton wanaweza kumsajili Eto’o kwa wakati ili aweze kucheza mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya timu yake ya zamani Chelsea Jumamosi hii. Everton tayari wameshamsajili Romelo Lukaku kwa ada ya paundi milioni 28 kutoka Chelsea kiangazi hiki na pia kumchukua Christian Atsu kwa mkopo kutoka hapohapo Chelsea. Mkataba wa Eto’o na Chelsea ulimalizika mwanzoni mwa Julai na kocha Jose Mourinho hakumuongeza mkataba mwingine. Eto’o ambaye amewahi kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Afrika mara nne, alifunga mabao 12 katika mechi 35 baada ya kusajiliwa na Chelsea kwa mwaka mmoja akitokea Anzhi Makhachkala Agosti mwaka jana.

No comments:

Post a Comment