Tuesday, August 26, 2014

GOMEZ AAPA KUPIGANIA NAFASI YAKE UJERUMANI.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Fiorentina ya Italia Mario Gomez ameapa kuwa atapigania nafasi yake katika kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani msimu huu. Nyota huyo wa zamani wa Bayern Munich alipatwa na majeraha mawili makubwa msimu uliopita na pamoja na kufanikiwa kurejea uwanjani kabla ya kumaliza kwa msimu wa 2013-2014, kocha wa Ujerumani Joachim Loew alimuacha katika kikosi cha kilichoshinda Kombe la Dunia nchini Brazil. Gomez tayari amekiri mara kadhaa kuwa ilikuwa ni jambo gumu kuishuhudia nchi yake huko Brazil bila uwepo wake lakini amesisitiza kuwa yote aliyokuwa akiwaza yanamlazimisha sasa alazimishe kurudi tena katika kikosi cha nchi hiyo kwa ajili ya michuano ya Ulaya 2016. Akihojiwa amesema suala la kurejea katika kikosi cha timu ya taifa lipo katika ndoto zake na ana matumaini makubwa kwamba atatizmiza malengo yake hayo.

No comments:

Post a Comment