Monday, August 25, 2014

VAN GAAL AKIRI ALAMA MOJA WALIYOPATA SUNDERLAND HAITOSHI.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Louis van Gaal amekiri baada ya kutoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Sunderland kuwa alama moja katika mechi mbili za Ligi Kuu walizocheza hazitoshi. Akihojiwa kocha huyo raia wa Uholanzi amesema wamepata alama moja na jambo hilo sio zuri kwa klabu kama hiyo. Van Gaal amesema wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii zaidi kwani wacchezaji wamesikitishwa na sare hiyo baada ya mchezo kwasababu walikuwa na uhakika wa kushinda. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa wanahitaji walau kushinda mechi moja ili kurejesha hali ya kujiamini halafu wataona huko mbele watakavyokwenda.

No comments:

Post a Comment