Tuesday, October 28, 2014

BALOTELLI AEPUKA ADHABU.

POLISI nchini Uingereza hawatachukua hatua yeyote dhidi ya Mario Balotelli kuhusu tuhuma za mshambuliaji huyo wa Liverpool kumtishia mwanamke aliyekuwa akipiga picha gari lake. Balotelli alituhumiwa kumfuata binti wa mama huyo wakati akipiga picha gari lake la kifahari la Ferrari. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na polisi wa jiji la Manchester, imedai kuwa hakuna tukio lolote uvunjifu wa sheria lililogunduliwa kutokana na tuhuma hizo. Kutoka na hilo jeshi hilo halitachukua hatua yeyote kwa Balotelli kuhusiana na tuhuma hizo. Tukio hilo lilitokea siku moja baada ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 kutolewa katika kipindi cha mapumziko wakati Liverpool ilipotandikwa mabao 3-0 dhidi ya Real Madrid katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki iliyopita. Balotelli ambaye alinunuliwa akitokea AC Milan kwa kitita cha paundi milioni 19 alishambuliwa kwa kubadilishana jezi na Pepe katika muda wa mapumziko.

No comments:

Post a Comment