Tuesday, October 28, 2014

TUTAINGA MKONO URUSI KW ASILIMIA 100 - BLATTER.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter amesema shirikisho hilo linaunga mkono Urusi kuwa mwenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na kupongeza maandalizi yake. Akihojiwa Blatter amesema bila kusita FIFA linaiunga mkono Urusi kwa asilimia 100 kuandaa michuano hiyo kwasababu wanaiamini serikali ya nchi hiyo. Vyanzo vya kidiplomasia vilidai mwezi uliopita kuwa mataifa ya Ulaya yanajadili kuunga mkono mpango wa Uingereza kumsusia rais wa Urusi Vladimir Putin michuano hiyo kwasababu ya vita vinavyoendelea mashariki mwa Ukraine. Blatter amesema hadhani kama taarifa hizo za kususia zitaleta tija yeyote kwani Urusi ni taifa kubwa na soka haliwezi kuinganosha nchi hiyo pekee bali dunia nzima.

No comments:

Post a Comment