Tuesday, October 28, 2014

WAJERUMANI WATAWALA ORODHA Y BALLON D'OR.

WACHEZAJI wa timu ya taifa ya Ujerumani ndio wametawala orodha ya kinyang’anyiro cha kutafuta Mchezaji Bora wa Mwaka wa Dunia inayojulikana kama Ballon d’Or. Katika orodha ya wachezaji 23, sita kati yao wametoka Ujerumani huku pia wakiteuliwa makocha 10 ambao nao watagombea tuzo ya kocha bora wa mwaka. Jurgen Klinsmann ni mmoja wa makocha walioteuliwa katika orodha hiyo baada ya kuingoza Marekani kutinga hatua ya timu 10 bora katika Kombe la Dunia. Orodha hiyo ya makocha imezua maswali mengi baada ya kuachwa makocha kama Jorge Luis Pinto wa Costa Rica na Jose Pekerman wa Colombia ambao walizisaidia timu zao kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo. Mbali na hao pia wapo Jorge Sampaoli ambaye naye aliushangaza ulimwengu wakati akiongoza Chile na kuwangoa mabingwa watetezi Hispania na kutinga hatua ya mtoano smbamba na kocha wa Vahid Halilhodzic ambaye aliisaidia Algeria kufikia hatua hiyo. Kwa upande mwingine orodha ya makocha imewajumuisha Pep Guardiola wa Bayern Munich pamoja na timu yake kuishia nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa msimu uliopita kwa kutandikwa na Real Madrid mabao 4-0, pamoja na Jose Mourinho pamoja na Chelsea kushindwa kunyakuwa taji lolote msimu uliopita. Nyota wa Ujerumani waliojumuishwa katika orodha hiyo nia pamoja na Manuel Neuer, Thomas Mueller, Toni Kroos, Mario Goetze, Philipp Lahm and Bastian Schweinsteiger wakati Argentina waliomaliza katika nafasi ya pili katika michuano ya Kombe la Dunia wao wakiingiza wacheza wachezaji watatu akiwemo Lionel Messi, Angel Di Maria and Javier Mascherano.

Orodha kamili ya wachezaji na nchi wanazotoka: Mario Goetze (Ujerumani) Toni Kroos (Ujerumani) Philipp Lahm (Ujerumani) Thomas Mueller (Ujerumani) Manuel Neuer (Ujerumani) Bastian Schweinsteiger (Ujerumani) Angel Di Maria (Argentina) Javier Mascherano (Argentina) Lionel Messi (Argentina) Andres Iniesta (Hispania) Sergio Ramos (Hispania) Diego Costa (Hispania) Karim Benzema (Ufaransa) Paul Pogba (Ufaransa) Gareth Bale (Wales) Eden Hazard (Ubelgiji) Thibaut Courtois (Ubelgiji) Cristiano Ronaldo (Ureno) Zlatan Ibrahimovic (Sweden) Neymar (Brazil) Arjen Robben (Netherlands) James Rodriguez (Colombia) Yaya Toure (Ivory Coast)

Orodha ya makocha na timu wanazofundisha: Carlo Ancelotti (Real Madrid) Antonio Conte (Italy/Juventus FC) Pep Guardiola (Bayern Munich) Juergen Klinsmann (Marekani) Joachim Loew (Ujerumani) Jose Mourinho (Chelsea) Manuel Pellegrini (Manchester City) Alejandro Sabella (Argentina) Diego Simeone (Atletico Madrid) Louis van Gaal (Uholanzi)

No comments:

Post a Comment