Tuesday, October 28, 2014

JEZI NAMBA MOJA YA ORLANDO PIRATES YAFUNGIWA KWA HESHIMA YA MEYIWA.

KATIKA kumkumbuka nahodha wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Bafana Bafana Senzo Meyiwa, mwenyekiti wa klabu ya Orlando Pirates Irvin Khoza ametangaza kuipumzisha jezi namba moja ya timu hiyo. Khoza amesema hadhani kama kuna mtu yeyote anayeweza kuziba nafasi ya Meyiwa ndio maana wameamua jezi yake kutovaliwa na yeyote tena. Meyiwa mwenye umri wa miaka 27 alipigwa risasi na kufariki dunia wakati akimtembelea mpenzi wake huko Vosloorus, Ekurhuleni Jumapili usiku. Huyo anakuwa mchezaji wa pili wa kupewa heshima hiyo baada ya jezi namba 22 iliyokuwa ikitumiwa na mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo Lesley Manyathela kusimamishwa kwa heshima yake baada ya kufariki kwa ajali ya gari mwaka 2003. Meyiwa alikuwa akitarajiwa kuingoza Pirates katika mchezo wa nusu fainali wa Kombe la Ligi ambao ungewakutanisha na mahasimu wao wa jiji la Soweto Kaizer Chiefs Jumamosi hii lakini umehahirishwa kutokana na kifo hicho. Badala yake Jumamosi hii kutafanyika mazishi ya golikipa huyo nyumbani kwao Umlazi jijini Durban.

No comments:

Post a Comment