Tuesday, October 28, 2014

HATIMAYE TEVEZ AITWA TENA ARGENTINA.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Juventus, Carlos Tevez ameteuliwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Argentina kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka mitatu. Tevez mwenye umri wa miaka 30 ameitwa katika kikosi hicho cha Gerardo Martino kwa ajili ya michezo ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Croatia na Ureno baada ya kuachwa na kocha wa zamani wa timu hiyo Alejandro Sabella toka mwaka 2011 mpka mwaka huu. Mara ya mwisho Tevez kuitumikia nchi yake ilikuwa katika robo fainali ya michuano ya Copa Amerika mwaka 2011 wakati Argentina walipong’olewa katika hatua ya hiyo baada ya golikipa wa Uruguay Fernando Muslera kuzuia penati ya mchezaji huyo. Tevez ameanza msimu wa Serie A kwa kiwango kikubwa akiwa ameifungia Juventus mabao sita na mawili zaidi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Nyota huyo pia amefunga mabao 13 katika mechi 64 alizoitumikia nchiyake kati ya mwaka 2004 mpaka 2011. Argentina inakabiliwa na mchezo dhidi ya Croatia utakaofanyika jijini London, Novemba 12 utakaofuatiwa na mchezo dhidi ya Ureno jijini Manchester siku sita baadae.

No comments:

Post a Comment