Wednesday, October 29, 2014

BALOTELLI ATOA GUNDU.


MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Liverpool Mario Balotelli jana alitoa gundu na kufanikiwa kuisaidia timu yake hiyo kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Ligi. Nyota huyo alitokea benchi na kufanikiwa kuisawazishia timu yake bao kabla ya Dejan Lovren hajaongeza lingine na kuiwezesha timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Swansea City. Kwa mujibu wa kocha msaidizi, Colin Pascoe, Balotelli alijiumiza wakati wakifanya mazoezi ya kupasha katika mchezo huo na kulazimika kumuona daktari kabla ya mchezo huo. Nyota huyo wa kimataifa wa Italia amekuwa akikosolewa kwa tabia yake pamoja na ukame wa kufunga mabao toka atue Anfield akitokea AC Milan Agosti mwaka huu.

No comments:

Post a Comment