Wednesday, October 29, 2014

KLABU BINGWA YA DUNIA KUFANYIKA KAMA ILIVYOPANGWA - FIFA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limedai kuwa maandalizi kwa ajili ya michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia itakayofanyika nchini Morocco itaendelea kama ilivyopangwa pamoja na wasiwasi juu ya mlipuko wa ugonjwa wa Ebola. Michuano hiyo ya siku 10 ambayo itashirikisha bingw wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya Real Madrid inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 10 mwaka huu. FIFA imesema imefanya mawasiliano na mamlaka husika nchini Morocco na kupokea ushauri kutoka kwa Shirika la Afya Duniani-WHO mara kwa mara kuhusiana na suala hilo. Morocco pia inatarajiwa kuwa mwenyeji wa michuano ya Mataifa ya Afrika Januari mwakani. Katika taarifa yake FIFA imedai kuwa afya za wachezaji, maofisa na mashabiki wa soka ni jambo wanalolipa kipaumbele kama ilivyo kwa michuano yeyote ya kimataifa ya FIFA. Kwa mujibu wa taarifa ya WHO, Morocco haijpata mgonjwa yeyote wa Ebola hivyo maandalizi yanaweza kuendelea kama yalivyopangwa. Mlipuko wa Ebola katika nchi za Afrika Magharibi umeambukiza zaidi ya watu 10,000 na kuua zaidi 5,000 kwa mujibu wa takwimu za WHO.

No comments:

Post a Comment