Monday, October 27, 2014

BLATTER ATUMA SALAMU ZAKE RAMBIRAMBI KWA NAHODHA WA AFRIKA KUSINI ALIYEUAWA.

RAIS wa Shirikisho la Soka la Dunia-FIFA, Sepp Blatter ametuma salamu zake za rambirambi kufuatia kifo cha golikipa na nahodha wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Senzo Meyiwa. Meyiwa mwenye umri wa miaka 27 alipigwa risasi na kufariki wakati akijaribu kumlinda mpenzi wake Kelly Khumalo wakati walipovamiwa na majambazi nyumbani kwa mwanadada huyo ambayo ni mwanamuziki. Kwa mujibu wa taarifa za polisi nchini nchini humo majambazi hayo yalikuwa yakitaka simu na vitu vya thamani vilivyokuwepo nyumbani kwa Khumalo, na kuongeza kuwa golikipa huyo alifariki mara tu baada ya kufikishwa hospitalini. Katika barua yake kwa rais wa Chama cha Soka cha Afrika Kusini, Danny Jordaan, Blatter alitum salama zake hizo kwa niaba ya jumuiya ya soka ya kimataifa kufuatia kifo hicho cha Meyiwa ambaye pia alikuwa golikipa namba moja wa klabu ya Orlando Pirates. Blatter aliongeza kwa majonzi makubwa Meyiwa atakumbukwa kwa wachezaji wenzake na mashabiki wa klabu na timu ya taifa na kuwataka familia na jamaa wa karibu na subira katika kipindi hiki kigumu. Meyiwa alikuwa akikaa langoni ktika mechi nne za mwisho za Afrika Kusini walizocheza kwa ajili ya kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mwakani na kufanikiwa kutofungwa bao hata moja katika mechi hizo. Nyota huyo pia aliisaidia timu ya Pirates kutinga hatua ya fainali ya Kombe la Ligi nchini humo. Kitita cha randi 250,000 sawa na dola 23,000 kimetolewa kwa yeyote atakayetoa taarifa kuhusu majambazi hayo.

No comments:

Post a Comment