Monday, October 27, 2014

POGBA AJIFANANISHA NA YAYA TOURE.

KIUNGO wa klabu ya Juventus, Paul Pogba amefananisha aina ya uchezaji wake nay a nyota wa klabu ya Manchester City Yaya Toure. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa alisaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Serie A ambao utamalizika mwaka 2019 Ijumaa iliyopita baada ya kuwa mchezaji muhimu kwa timu hiyo na nchi yake toka alipotua jijini Turin akitokea Manchester United kama mchezaji huru miaka miwili iliyopita. Meneja wa Juventus, Massilimiano Allegri amesema mwishoni mwa wiki kuwa Pogba bado ana kazi kubwa ya kufanya ili aweze kuja kuwa mchezaji bora wa dunia. Akihojiwa na mtandao wa FIFA.com, Pogba amesema anadhani bado kuna wachezaji wengi bora zaidi yake lakini atajitahidi kadri awezavyo ili afikie ubora unaotakiwa. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kuna wachezaji wengi wa nafasi ya kiungo ambao anawahusudu akimtolea mfano Toure ambaye ana umbo na nguvu sawa kama yeye lakini amezidi uzoefu.

No comments:

Post a Comment