Monday, October 27, 2014

WAENDESHA MASHITAKA KUKATA RUFANI HUKUMU YA PISTORIUS.

WAENDESHA mashitaka nchini Afrika Kusini wamedai kuwa watakata rufani dhidi ya hukumu aliyopewa mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius kwa kumuua mpenzi wake. Wiki iliyopita Pistorius alianza kutumikia adhabu yake ya miaka mitano jela aliyopewa kwa kosa kumuua bila kukusudia mpenzi wake Reeva Steenkamp ingawa anaweza kuachiwa katika kipindi cha miezi 10. Msemaji wa waendesha mashitaka hao amesema rufani hiyo itaegemea zaidi kuhoji vipengele vya sheria vilivyotumika kutoa hukumu hiyo. Familia ya mwanariadha huyo wenyewe wamesema hawatakata rufani kupinga adhabu aliyopewa mtoto wao. Pistorius pia alipewa adhabu ya kufungiw kutumia silaha kwa kipindi cha miaka mitatu kwa kufyatua risasi katika mgahawa.

No comments:

Post a Comment