Tuesday, October 28, 2014

NIGERIA YAKABILIWA NA TISHIO LA KUFUNGIWA MICHUANO YA KIMATAIFA.

NIGERIA inakabiliwa na tishio lingine la kufungiwa michuano ya kimataifa yakiwemo yale ya Mataifa ya Afrika yatakayofanyika mapema mwakani. Hatua inakuja kufuatia uamuzi wa mahakama kuu kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Shirikisho la Soka nchini humo-NFF. Mahakama kuu ya Jos ilifutilia mbali uchanguzi wa Amaju Pinnick kuwa rais wa shirikisho hilo. Hii ni mara ya pili Nigieria kupigwa marufuku kwa sababu ya serikali kuingilia masuala ya shirikisho hilo. Shirikisho la soka Duniani-FIFA limetoa onyo kuwa kuingiliwa kwa masuala ya soka kutasababisha Nigeria kupigwa marufuku hadi Mei mwakani.

No comments:

Post a Comment