Wednesday, October 29, 2014

CHELSEA CHUPUCHUPU KWA KITIMU CHA DARAJA LA PILI.

KLABU ya Chelsea jana imefanikiwa kupata bao katika dakika za mwisho kuepuka aibu ya kufungwa na timu ya daraja la pili ya Shrewbury na kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Ligi. Kikosi cha Chelsea kilionekana kuhangaika kucheza vizuri katika nyasi zilizolowa za Uwanja wa Greenhous Meadow lakini walifanikiwa kupata bao la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji wao mahiri Didier Drogba katika dakika ya 48 ya mchezo huo. Hata hivyo wenyeji walisawazisha bao hilo katika dakika ya 77 kupitia kwa Andy Mangan na kupelekea mchezo huo kuwa mgumu lakini katika dakika ya 81 Shrewsbury walijikuta wakijifunga bao kupitia kwa Jermaine Grandison aliyekuwa katika harakati za kuokoa. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo kocha wa Shrewbury Micky Mellon aliwapongeza wachezaji wake kuonyesha mchezo mzuri na kuwapa wakati mgumu wapinzani wao pamoja na tofauti kubwa kati yao zilizopo. Kwa upande wa meneja wa Chelsea Jose Mourinho alikiri kuwa na wasiwasi wakati wapinzani wao waliposawazisha lakini alimpongeza Drogba kwa kuonyesha kiwangi kikubwa ambacho kilisaidia wao kuibuka na ushindi huo muhimu.

No comments:

Post a Comment