Wednesday, October 29, 2014

MARTINS AONGEZWA MKATABA NA SOUNDERS.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Nigeria, Obafemi Martins amesaini mkataba mpya na klabu ya Seattle Sounders inayoshiriki Ligi Kuu ya Marekani. Pamoja na maafikiano katika mkataba huo kutowekwa wazi, Martins amekuwa akitarajiwa kupewa mkataba mpya kutokana na kiwango kikubwa alichoonyesha. Meneja wa klabu hiyo Adrian Hanauer alithibitisha Martins kusaini mkataba huo wa kuendelea kuitumikia timu hiyo aliyojiunga nayo mwaka jana. Msimu huu Martins amefanikiwa kuifungia Sounders mabao 17 na kusaidia mengine 13 na kusaidia kushinda taji la Ngao ya Mashabiki pamoja na Kombe la Wazi la Marekani.

No comments:

Post a Comment