Friday, October 24, 2014

ENYEAMA ATAKA CAF KUSITISHA AFCON.

GOLIKIPA na nahodha wa timu ya taifa ya Nigeria maarufu kama Super Eagles, Vincent Enyeama amelitaka Shirikisho la Soka la Afrika-CAF kusitisha michuano ya Mataifa ya Afrika-AFCON inayotarajiwa kufanyika Januari mwakani. Enyeama ambaye anakipiga katika klabu ya Lille amefafanua kuwa michuano hiyo inapaswa kusitishwa kutokana na wasiwasi juu ya ugonjwa wa Ebola kuongezeka. Golikipa huyo mwenye umri wa miaka 32 ameeleza woga wake kuwa ugonjwa huo ambao umeshaua zaidi ya watu 4,500 mpaka sasa utasambaa zaidi kufuatia mkusanyiko wa watu watakaokuwepo viwanjani. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa hatari ni kubwa kama AFCON itaandaliwa wakati huu ambapo bado ugonjwa huo haujadhibitiwa lakini amesema atashiriki kama nchi yake itafuzu michuano hiyo pamoja na hatari iliyopo.

No comments:

Post a Comment