Friday, October 24, 2014

WACHEZAJI WA BAYERN WATEMBELEA KITUO CHA WAKIMBIZI.

WACHEZAJI wa klabu ya Bayern Munich, wametembelea kituo cha wakimbizi kilichopo kaskazini mwa Ujerumani katika kipindi hiki ambacho nchi hiyo inakabiliwa na ongezeko la watu wengi wanaohitaji msaada. Wachezaji hao akiwemo Bastian Schweinsteiger na Holger Badstuber walitembelea kituo hicho ambacho kina mayatima 250 ambao hawana wazazi wala ndugu juzi baada ya timu hiyo kurejea kutoka Roma ambako pia walimtembelea Papa Francis huko Vatican. Rais wa klabu hiyo Karl-Heinz Rummenigge aliyeongoza ujumbe huo na kutoa msaada wa nguo na vifaa vya michezo amesema watoto hao hawana chopchote zaidi ya nguo walizovaa hivyo anadhani wana jukumu la kuwasaidia wao na wengine. Mwaka huu Ujerumani inategemea zaidi watu 200,000 wanaotafuta makazi katika mipaka yake kuzunguka nchi ikiwa ni ongezeko la asilimia 60 kulinganisha na mwaka jana. Makazi mapya ya wakimbizi yametengenezwa kuzunguka nchi ikiwemo kambi za zamani za jeshi na shule ili kuweza kukabiliana na ongezeko hilo la wakimbizi wengi wao wakiwa wametoka katika nchi za Syria na Iraq.

No comments:

Post a Comment