Monday, October 27, 2014

LENGO LA MILAN NI KUCHEZA LIGI YA MABINGWA ULAYA MSIMU UJAO - DE JONG.

MCHEZAJI nyota wa AC Milan, Nigel de Jong amesisitiza kuwa suala la kupata nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya bado lipo katika malengo yao kufuatia kung’ang’aniwa sare ya bao 1-1 nyumbani dhidi ya Fiorentina jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi aliifungia Milan bao la kuongoza kabl ya mapumziko lakini Josip Ilicic alivuruga sherehe yao kwa kusawazisha bao hilo katika kipindi cha pili. De Jong amesema Fiorentina walipata nafasi moja lakinib aliitumia vyema ila kwa upande walionekana kuchoka ndio maana wakaambulia alama hiyo moja. De Jong aliendelea kudai kuwa pamoja na hayo bado hawajakata tamaa katika kuhakikisha wanamaliza katika nafasi tatu za juu ambazo zitawapa tiketi ya kushiriki michuano hiyo mwakani. Kwasasa Milan wako katika nafasi ya sita katika msimamo wa Serie A wakiwa na alama 15 katika mechi nane walizocheza.

No comments:

Post a Comment