Monday, October 27, 2014

VIJEBA VYAIPONZA GHANA U-17.

TIMU ya taifa ya Ghana ya vijana chini ya umri wa miaka 17 imeondolewa katika michuano ya vijana wa umri huo mwakani kwasababu ya kudanganya umri. Timu hiyo inayojulikana kama Black Starlets iliitandika Cameroon katika mechi zao mbili za kufuzu michuano hiyo itakayochezwa Niger lakini nchi hiyo iliituhumu Ghana kwa kudanganya umri kwa baadhi ya wachezaji wake. Chama cha Soka cha Ghana-GFA kimethibitisha kupata barua kutoka Shirikisho la Soka la Afrika-CAF ya kuenguliwa baada ya kuthibitika kuwa tuhuma hizo za kudanganya umri zilikuwa za kweli. Cameroon walipeleka malalamiko yao dhidi ya wachezaji saba wa Ghana baada ya kufungwa mabao 2-1 katika mchezo wao mkondo wa kwanza. Kamati ya kitabibu ya CAF ilitoa taarifa ya uchunguzi wake kuhusu tuhuma hizo kuwa kuthibitisha kuwa ni kweli wachezaji hao walizidi umri lakini Ghana wenyewe wamesema watapinga uamuzi huo.

No comments:

Post a Comment