Monday, October 27, 2014

ZIDANE NI MFALME WA SOKA - MOURA.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG Lucas Moura amesema nyota wa zamani wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa Zinedine Zidane ndiye mfalme wa soka. Zidane mwenye umri wa miaka 42 amewahi kushinda Kombe la Dunia, michuano ya Ulaya, mataji mawili ya Serie A akiwa na Juventus na taji moja la ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Madrid huku pia akitunukiwa tuzo ya Ballon d’Or mwaka 1998. Winga huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 22 amesema kupata nafasi ya kukutana na Zidane ililikuwa kama ndoto kwake kwani ndiye anayemhusudu sana toka akiwa mdogo. Moura amesema kwake Zidane ndiye mfalme wa soka na siku zote amekuwa akitamani kufikia mafanikio yake.

No comments:

Post a Comment