Monday, November 24, 2014

APPIAH NJIANI KUCHUKUA MIKOBA YA KUINOA AL KHARTOUM.

KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah anatarajiwa kufikia makubaliano ya kuinoa klabu ya soka ya Al Khartoum ya Sudan. Vyombo vya habari nchini Sudan vimedai kuwa klabu hiyo tayari imeshamaliza mazungumzo na kocha huyo ambaye aliingoza Ghana katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil. Appiah mwenye umri wa miaka 54 alitimuliwa na Shirikisho la Soka la nchi yake Septemba mwaka huu na sasa amesaini mkataba wa awali wa makubaliano hayo. Taarifa za ndani zinadai kuwa Appiah alitumia siku mbili jijini Khartoum kukamilisha dili hilo ambalo litamuwezesha kupokea kitita cha dola 39,000 kwa mwezi. Klabu ya Al Khartoum ambayo inamilikiwa na jeshi la Sudan ilimaliza katika nafasi ya nne msimu uliopita na wanatarajiwa kushiriki michuano ijayo ya Kombe la Shirikisho.

No comments:

Post a Comment