Monday, November 24, 2014

GYAN ABAINISHA YUKO FITI.

NAHODHA wa timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan amebainisha kuwa yuko fiti baada ya kupita michezo miwili ya kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon mwakani. Kabla ya michezo hiyo dhidi ya Uganda na Togo, mshambuliaji huyo alikuwa akisumbuliwa na majeruhi yaliyomfanya kushindwa kucheza. Akihojiwa Gyan amesema alikuwa akitamani sana kucheza mechi dhidi ya Togo lakini daktari alimwambia litakuwa jambo la hatari hivyo akashindwa kufanya hivyo. Hata hivyo nyota huyo amesema kwasasa anajisikia kuwa fiti tayari kuitumikia klabu yake ya Al Ain. Gyan aliifungia Ghana mabao matatu katika michezo ya kufuzu Afcon.

No comments:

Post a Comment