Monday, November 24, 2014

SCHUMACHER BADO ANA SAFARI NDEFU NA NGUMU KUELEKEA KUPONA KUFUATIA AJALI MBAYA ALIYOPATA.

MENEJA wa Michael Schumacher amesema bado hakuna muda kamili kwa nyota huyo wa zamani wa mashindano ya langalanga kupona kufuatia ajali mbaya aliyopata wakati akiteleza katika barafu karibu mwaka mmoja uliopita. Sabine Kehm amesema haiwezekani kujua ni muda gani haswa utachukua kwa Schumacher kupona kabisa kwani bado anakabiliwa na safari ndefu na ngumu kuelekea huko. Schumacher alipata majeraha ya kichwa wakati akiwa na familia yake katika mapumziko katika milima ya Ufaransa Desemba 29, ajali ambayo ilimuacha na majeraha ya ubongo yaliyomfanya kutojitambua kwa muda wa miezi sita. Kwasasa nguli huyo anajiuguza nyumbani kwake huko Gland, Switzerland toka Juni mwaka huu. Kehm amesema Schumacher anaendelea vyema lakini bado ana kipindi kirefu na kigumu ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.

No comments:

Post a Comment