Monday, November 24, 2014

CRUZEIRO YANYAKUWA TAJI LA PILI MFULULIZO LIGI KUU NCHINI BRAZIL.

KLABU ya Cruzeiro imefanikiwa kunyakuwa ubingwa wa Ligi Kuu nchini Brazil kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuitandika Goias kwa mabao 2-1 jana. Mabao yaliyofungwa na kiungo Ricardo Goulart na Everton Ribeiro yalitosha kuihakikishia timu hiyo ubingwa wake wa nne wa ligi huku kukiwa kumebaki michezo miwili kabla ya ligi kumalizika. Matokeo hayo mbele ya mashabiki karibu 60,000 waliohudhuria mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Mineirao huko Belo Horizonte yamewahakikishia ubingwa huo baada ya Sao Paulo waliokuwa nafasi ya pili kufungwa na Santos kwa bao 1-0 huko Cuiaba. Cruzeiro inakuwa timu ya kwanza kushinda mataji mfululizo toka Sao Paulo walipofanya hivyo kuanzia mwaka 2006 mpaka 2008.

No comments:

Post a Comment