Monday, November 24, 2014

BLATTER ANAPSWA KUJIUZULU - RAUBALL.

RAIS wa Ligi ya Soka ya Ujerumani-DFL, Reinhard Rauball amedai kumwambia rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter kujiuzulu nafasi hiyo. Rauball alikaririwa na gazeti la Kicker akidai kuwa anadhani wakati wa Blatter kuachia nafasi hiyo umefika kutokana na kashfa mbalimbali ambazo zimeendelea kuliandama shirikisho hilo. Kashfa ambayo inaiandama shirikisho hilo kwasasa ni kuhusu ripoti ya uchunguzi ya Michael Garcia yenye kurasa 430 ambayo FIFA imegoma kuichapisha kwa kuogopa kukiuka sheria. Rauball amesistiza kuwa kashfa hiyo inayohusu mchakato wa kutafuta weneywe wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na 2022 inapaswa kumpelekea Blatter kujiuzulu ili kulinda heshima ya michuano hiyo. Rauball alifafanua kuwa jambo hilo kabla ya kuzungumza na vyombo vya habari alimpigia simu Blatter na kumueleza mawazo yake kuhusiana na hilo.

No comments:

Post a Comment