Monday, November 24, 2014

REUS NJE MPAKA JANUARI.

KIUNGO wa klabu ya Borussia Dortmund, Marco Reus anatarajiwa kukaa nje ya uwanja mpaka Januari mwakani baada ya kuchanika msuli katika kifundo chake cha mguu wa kulia wakati wa mchezo dhidi ya Paderborn ambao ulimazika kwa sare ya mabao 2-2 Jumamosi iliyopita. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 25 alikoza michuano ya Kombe la Dunia ambapo nchi yake ya Ujerumani ilinyakuwa taji hilo kutokana na matatizo ya kifundo cha mguu na baadae mwanzoni mwa msimu alikosa michezo saba ya klabu yake kwa matatizo kama hayo. Nyota aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter akiwashukuru mashabiki wake kwa kumtakia heri ya kupona mapema na kudai kuwa atarejea akiwa imara zaidi. Dortmund ambao msimu uliopita walimaliza katika nafasi ya pili katika msimamo wa Bundesliga kwasasa wanashika nafasi ya tatu kutoka mkiani wakiwa wameshinda mechi tatu pekee kati ya 12 walizocheza.

No comments:

Post a Comment