Monday, November 24, 2014

NATAKA KUWA BORA KAMA ZIDANE - POGBA.

KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Ufaransa, Paul Pogba amebainisha kuwa anataka kuwa bora kama Zinedine Zidane, huku akidai Juventus ni klabu kubwa kama ilivyo Real Madrid. Pogba amekuwa akifananishwa na Yaya Toure na Patrick Vieira kutokana na aina yake ya mchezo lakini mwenyewe amesema kuna mchezaji mwingine ambaye anapenda kufikia mafanikio yake ambaye ni Zidane. Akihojiwa kuhusiana na tetesi za kuhamia nchini Hispania, Pogba amesema anadhani Madrid ni klabu kubwa kama ilivyo kwa Juventus, kwani alikuwa Manchester United lakini bado aliamua kujiunga na timu hiyo ya Turin. Pogba amesema anajisikia vyema nchini Italia kwani kila mtu amekuwa kama sehemu ya familia katika klabu hiyo, jambo pekee analofikiria ni kuimarika kama mchezaji na ni matumaini yake atafikia mafanikio ya Zidane.

No comments:

Post a Comment