Friday, November 28, 2014

CONFEDERATION CUP FAINAL 2014: SEWE SPORT KUONYESHANA KAZI NA AL-AHLY.

KLABU ya Al-Ahly inatarajia kujitupa uwanjani mwishoni mwa wiki hii katika mchezo wa fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya klabu ya Sewe Sport ya Ivory Coast. Al-Alhy itaingia katika mchezo huo kutafuta ushindi kwa udi na uvumba ili kurejesha heshima ya soka la Misri ambalo katika siku za karibuni linaonekana kuporomoka. Sewe Sport itaikaribisha Al-Ahly katika mchezo wa mkondo wa kwanza utakaofanyika jijini Abdijan kesho huku mchezo wa marudiano ukitarajiwa kuchezwa Desemba 6 jijini Cairo. Baada ya miongo kadhaa ya mafanikio katika soka kwa timu ya taifa na ngazi ya vilabu, mwaka huu umekuwa sio mzuri kwa nchi hiyo baada ya kushuhudia timu ya taifa ikishindwa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika na vilabu kushindwa kutamba katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment