Friday, November 28, 2014

ROY KEANE AACHIA NGAZI ASTON VILLA.

KLABU ya Aston Villa imetangaza kuwa Roy Keane amejiuzulu wadhifa wake wa kocha wa msaidizi wa timu hiyo. Mapema Keane alikaririwa akidai kuwa anapata tabu kuhudumia vibarua viwili alivyokuwa navyo. Keane ambaye pia ni kocha msaidizi wa Ireland amesema sio haki kwa pande zote mbili, hivyo anatakiwa kufanya uamuzi wa kuchagua kibarua kimoja. Kocha wa Villa Paul Lambert alithibitisha asubuhi ya leo kuwa taarifa hizo na kudai kuwa ana heshimu uamuzi uliochukuliwa.

No comments:

Post a Comment